Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

Labels

Thursday, December 14, 2017

Rais wa Zimbabwe Munangagwa aongoza mkutano wa kwanza wa kamati kuu ya chama baada ya Mugabe kujiuzulu.

Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ameongoza mkutano wa wake wa kwanza wa kamati kuu ya chama cha ZANU-PF, baada ya rais wa zamani Robert Mugabe kujiuzulu wiki tatu zilizopita.

Mkutano huo uliofanyika kwenye makao makuu ya ZANU PF umeashiria mwanzo wa mkutano mkuu wa kawaida wa siku moja wa chama uliopangwa kufanyika kesho.

Ajenda za mkutano mkuu huo ni pamoja na kumthibitisha Bw. Mnangagwa kuwa rais na katibu mkuu wa ZANU-PF, kutambuliwa kwake kama mgombea urais wa chama hicho katika uchaguzi utakaofanyika mwaka kesho, na kuidhinisha kuwafukuza wanachama wanaosemekana kuwa kundi la G40 la mke wa rais wa zamani Bibi Grace Mugabe. @cri

0 comments:

Post a Comment