Showing posts with label BURUDANI. Show all posts
Showing posts with label BURUDANI. Show all posts
Monday, November 13, 2017
Wednesday, November 1, 2017
Aslay avuta ndinga mpya itizame hapa.
"Alhamdulillah Asantee Mungu kwa hiki ulichonipa naishukuru management yangu Chambusso na Mxcarter, nakupenda Mama yangu kokote ulipo kila hatua dua 'new car' Umma unaongea" alindika Aslay kupitia mtandao wake wa Facebook.
Aslay Isihaka kwa mara ya kwanza kuanza kumiliki gari yake alizawadiwa na uongozi wake wa kwanza wa Yamoto Band chini ya Mkubwa Fella katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake mwaka 2015
Tuesday, October 31, 2017
Alichokiandika Jaguar baada ya Uhuru Kenyatta kutangazwa Rais wa Kenya.
Msanii Jaguar wa Kenya na pia Mbunge wa jimbo la Starehe County ya mjini Nairobi kupitia muungano wa chama cha Jubilee, amempongeza Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa tena katika kiti cha Urais katika uchaguzi wa marudio ambao umefanyika wiki iliyopita.
Kupitia mtandao wa Twitter, Jaguar ameandika, “Congratulations @UKenyatta on your reelection. I thank all who voted and equally expressed their democratic right. Let’s maintain peace.”
Congratulations @UKenyatta on your reelection. I thank all who voted and equally expressed their democratic right. Let's maintain peace. pic.twitter.com/oI05f6CZLa— Hon. Jaguar (@RealJaguarKenya) October 30, 2017
Rais Kenyatta alitangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho na Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo (IEBC), Wafula Chebukati kupata kura 7,483,895 sawa na asilimia 98, mpinzani wake Raila Odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa naasilimia 0.96.
Jumla ya wananchi 7,616,217 walipiga kura katika uchaguzi huo kati ya watu milioni 19.6 waliojiandikisha kupiga kura.
Wednesday, October 25, 2017
Shahidi afichua mapya ya Kanumba
Kesi inayomkabili Muigizaji Elizabeth Michael 'Lulu', imeendelea leo
katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambapo ushahidi wa upande wa
utetezi uliokuwa ukisubiriwa umewasilishwa na kusomwa na Polisi
Detective Sergeant Nengea aliyerekodi.
ushahidi huo kutoka kwa aliyekuwa Daktari wa Marehemu Steven Kanumba.
Katika ushahidi uliosomwa na Sergeant
Nengea (ambaye mahakama imemtambua kama shahidi) ambao aliurekodi kutoka
kwa Josephine Mushumbusi umedai kwamba "Marehemu alikua na matatizo ya
damu, upungufu wa hewa kwenye ubongo, alikuwa anasikia maumivu katika
ubongo na akili kuchoka".
Aidha ushahidi huo umekamilisha kesi
hiyo siku ya leo lakini Wakili Kibatala ameiomba mahakama kumruhusu
kumpatia nafasi ya kutoa hoja za ziada ambazo zitasaidia katika kufanya
maamuzi juu ya kesi hiyo.
Hata hivyo Jaji Sam Rumanyika amesema
kesho wazee wa baraza watakaa na kujadili kama Lulu ana hatia katika
kesi hiyo inayomkabili au hana, na kusubiria kupanga siku ya hukumu.