Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

HABARI KWA WAKATI KUTOKA HAPA

Tunakuhakikishia kupata habari zote zilizo muhimu kutoka ulimwenguni kote kwa wakati, unaweza kusubscribe mtandao wetu na ukawa unapokea habari zote katika email yako punde tu tuchapishapo machapisho yetu. Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

HABARI ZA MICHEZO

Sasa African news tunakuhakikishia kupata taarifa zote za kimichezo kutoka viwanja mbalimbali duniani, lengo ni kuhakikisha hupitwi na lolote katika ulimwengu wa michezo.Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

TAARIFA ZA BURUDANI NA HABARI ZA WASANII

Unapenda masuala ya burudani? Ni jukumu letu kuhakikisha unazipata info zote za burudani na wasanii wanaokupa burudani, unapata video mpya, movie pamoja na muziki. Kaa karibu nasi.

KURASA ZA MAGAZETI KILA SIKU

Tunakupatia kila ambacho kinaandikwa katika magazeti ya Tanzania na nje ya Tanzania, usitie shaka ukishindwa kununua gazeti uipendalo, sogea karibu nasi na upate kila unachokihitaji.

MAHUSIANO

Fahamu mambo mengi katika ulimwengu wa mapenzi kwa kupitia dondoo, simulizi na visa mbalimbali kupitia Jim Media Online, Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

Labels

Showing posts with label MAHUSIANO. Show all posts
Showing posts with label MAHUSIANO. Show all posts

Monday, March 19, 2018

Jinsi ya kufanya ili mtoto apende chakula.


Wazazi wengi hasa waishio mijini wanakumbana na changamoto ya watoto wao kutopenda kula ama kwa kukosa hamu na hata vinginevyo. Tumepata wasaa wa kuzungumza na mtaalamu wa lishe kutoka Shirika la Chakula Dunia (WFP), Neema Shosho na hapa tutakupa machache juu ya nini ufanye mwanao apende kula.

Shosho anashauri kwamba wakati wa kumlisha mtoto ni vyema mzazi au mlezi utumie lugha ya upole na upendo ili kumuhamasisha mtoto kula. Lugha za matusi, vitisho na ukali humfanya mtoto achukie na akatae kula chakula.

Kwamba ili mtoto apende kula, pendelea kumpa chakula chake kipindi ambacho familia pia inakula. Hii itamuhamasisha kula zaidi. Asile peke yake mara zote. Hata hivyo kumlisha mtoto kunahitaji uvumilivu. Tenga muda wa kutosha wa kumlisha mtoto wako. Ongea nae, zunguka nae na cheza nae huku ukimbembeleza kula kwa upole na upendo

Kamwe usijaribu kumkaba mtoto ili ale chakula. Hii inaweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo chakula kupita njia ya hewa jambo linaloweza kugharimu uhai wake. Vilevile kumkaba koo kunaleta madhara ya kisaikolojia wakati mtoto ataona kula ni adhabu na kuchukia chakula.

Jaribu kumpa mtoto vyakula vya aina mbalimbali ili ujue anapenda vyakula gani. Kwa watoto wakubwa kidogo mfano miaka mitatu na kuendelea ni muhimu kumshirikisha mtoto katika uandaaji wa chakula. Muulize angependa kula nini? Zungumza naye kama inawezekana kuandaa anachotaka mwambie na kama haiwezekani ajue kwa nini. Usimkaripie. Unampotezea uwezo wa kujiamini na ujenzi wa hoja. Nenda na watoto wako eneo unalonunulia chakula (gengeni, sokoni, supermarket, dukani, gulioni) na uwasikilize nini wanapendelea kula. Kumbuka mnaweza kufanya machaguo sahihi ya vyakula kwa bei nafuu kabisa.

Wewe mzazi au mlezi uwe kioo kwa mtoto wako kwa kula mlo kamili na wa bora. Mzazi ukila mlo kamili na wa bora ni rahisi mtoto kuiga na kupenda mlo wake. Vilevile jitahidi vyombo unavyotumia kumlishia mtoto viwe vinavutia. Usiweke chakula kwenye bakuli lililoharibika mfano lililoungua, lenye ufa, lililopondeka na kadhalika. Nunua vyombo vya watoto vizuri, vyenye kuvutia na vya bei nafuu kabisa ili kumuhamasisha mtoto kula.

Watoto wakubwa waruhusiwe kuingia jikoni chini ya uangalizi wa mzazi au mlezi. Waonyeshe unavyoandaa chakula na washirikishe msaidiane kuandaa mlo kamili na ulio bora. Kumbuka kula mlo bora na kamili sio lazima uwe na pesa nyingi. Pangilia pesa uliyonayo na hakikisha unanunua vyakula bora, kamili na asili vinayopatikana kwenye eneo lako unaloishi

Alama 11 za mpenzi mwenye mchepuko.




Kila mmoja atakubaliana na mimi kwamba uhusiano baina ya wapendanao ulikusudiwa kuwa ya upendo, maelewano, kuaminiana na urafiki wa hali ya juu. Kwa bahati mbaya hali halisi siyo hiyo katika mahusiano ya wengi. Wengi wetu wameumizwa kwa mpenzi mmoja au mara nyingine wote kutokuwa waaminifu katika mahusiano yao.

Kutokuwa mwaminifu hapa namaanisha hali ya mpenzi mmoja kuwa na mahusiano yasiyo rasmi na mpenzi au wapenzi wengine pembeni au mchepuko kwa lugha ya kisasa

Japo jambo hili hufanyika kwa siri sana kwa kuogopa kuharibu mahusiano mtu aliyonayo, wako baadhi ambao wamegundulika na mahusiano yakaathirika kwa kiasi kikubwa na wengine yalikufa kabisa.

Wako ambao wameweza kuhimili machungu ya kugundua hali ya wapenzi wao kutokuwa waaminifu lakini pia wako ambao imewashinda kabisa kuwa wavumilivu, wako ambao hali hii imewaletea shida kihisia, kisaikolojia na hata kiafya.

Kwa bahati mbaya wengi wetu hatuzijui hata dalili au alama zozote za kutujulisha mabadiliko waliyonayo wapenzi wetu ili basi walao tuanze mapema kufanya uchunguzi au kupeana tahadhari kabla makubwa na machungu zaidi hayajatokea.

Zifuatazo nia alama zitakazokusaidia kuwa macho mara utakapoona mazingira ya kufanana nazo yanatokea katika uhusiano yenu, alama hizi nimezikusanya katika mazungumzo na baadhi ya watu niliowahi kusaidiana nao kutatua matatizo ya mahusiano yao na pia nikazihakikisha kupitia kusoma vitabu mbalimbali, kwa hiyo nina uhakika zitakusaidia kuona uhalisi wa mambo, na yamkini utaona baadhi ya alama ambazo umeshawahi kuzihisi au kuzishuhudia katika mahusiano yako.

Kuongezeka ghafla kwa hali ya kujipenda

Yawezekana mpenzi wako alikuwa amezoea kuvaa kawaida, hapa simaanishi kutopendeza, na wewe ulikuwa umemzoea katika hali fulani ya mavazi au mitindo mara ghafla anabadilika nakuwa mtanashati zaidi, ana badilisha mavazi, anapenda mavazi ya gharama, labda alikuwa hatumii manukato lakini ghafla anaanza kupenda manukato tena ya gharama, anakuwa mtu wa kujijali zaidi ya kawaida yake kiasi ambacho hukumzoea. Katika hali hii jaribu kuwa macho zaidi kufahamu nini kilicho sababisha mabadiliko ya ghafla kiasi hicho.

Kuanza kuchelewa kutoka kazini mara kwa mara

Sio kwamba kila mtu anapochelewa kutoka kazini basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini wewe ni shahidi wa hili.

Unaweza kukuta mtu alikuwa anafanya kazi hiyo muda mrefu tu tangia muanze mapenzi yenu, mara ghafla hali inabadilika, sikuhizi anachelewa sana kurudi nyumbani, na anaporudi unaweza kutegemea utamwona amechoka kimwili na hata kiakili kwa majukumu ya kazi kuhusiana na asili ya kazi anayoifanya lakini unakuta mtu wala haonyeshi kuchoka, ana furaha kama kawaida.

Hali hii inapojitokeza mara kwa mara usichelewe kufungua macho na kudadisi mazingira maana yamkini ni kweli amepata kazi ya ziada ila siyo ile ya ajira unayoijua wewe.

Kupenda kutembea na mipira ya kinga “condoms”

Inashangaza mara nyingine kusikia mpenzi mmoja ana tabia ya kubeba kondomu kwenye pochi yake au mfukoni kwa kisingizio kuwa anajali, cha kushangaza zaidi unakuta yuko katika mahusiano na mkewe au mumewe. Yamkini ni kweli kunakujali na labda katika mahusiano yenu hili sio la kushtua kwa sababu mnajali afya zenu au mnatumia kondomu kwa sababu zaidi ya moja, lakini inakuwaje pale unapogundua kuwa ile kondomu uliyokuwa unaiona haipo tena na yamkini wewe hukuhusika katika kuitumia.

Mazingira tatanishi ya simu

Inawezekana mpenzi wako sio mtu wa kupokea simu au kupiga simu sana, na hivi ndiyo ulivyomzoea, mara ghafla simu zinaanza kumiminika mpaka mida ya usiku. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza ichukua na kumpatia lakini ghafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu yake, nimeongea na wengine ambao wanakwenda na simu hadi bafuni isije ikasikika.

Wengine wameanza kuondoa milio katika simu zao wakati haikuwa kawaida yao, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kuzipokea na kuongea kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya anaongea kiuaminifu kabisa lakini mtu uliyempenda na ukamzoea unaweza kugundua uhalisi wa anachokiongea kwenye simu na jinsia ya anayeongea naye kwa kumuangalia usoni tu.

Yamkini mpenzi wako amepigiwa simu na kwa sababu hakuwepo karibu ukaipokea, na mara mpigaji wa simu anapogundua aliyepokea sio mwenye simu anakata simu hiyo ghafla, au ghafla unagundua kila simu inayopigwa kwenye simu ya mpenzi wako haionyeshi namba au haionyeshi jina. Mazingira kama haya yanapozidi basi jaribu kuchukua hatua, yawezekana kuna mvamizi tayari katika mahusiano yenu.


Itaendelea

Tuesday, January 9, 2018

Umuhimu wa Kumpunguzia Mtoto Shinikizo la Kufaulu


Ufaulu wa mitihani umepewa nafasi ya pekee katika mfumo wetu wa elimu. Shule zetu, kwa hakika, hazina namna nyingine ya kumwelimisha mtoto zaidi ya kumtaka akusanye, akumbuke na kutumia maarifa aliyonayo kujibu maswali ya mtihani.

Ingawa ustawi wa jumla wa mwanadamu hautegemei eneo hilo moja la ukusanyaji na utumiaji wa maarifa, shule zetu zinaonekana kuamini pasipo mtu kuwa na maarifa mengi hawezi kufanikiwa.

Kasumba hii imetuathiri na sisi wazai. Tunafikiri, kwa mfano, ni lazima mtoto afaulu masomo kwa kiwango cha juu ili afanikiwe. Matarajio haya makubwa yanatufanya tuwaweke watoto kwenye shinikizo kubwa mno la kufaulu tukiamini ufaulu huo ndio kigezo cha ustawi wao katika maisha.

Matokeo yake, tangu mtoto anapoingia shuleni kwa mara ya kwanza mpaka anamaliza, anajikuta katika mazingira ambayo kimsingi hana kazi nyingine zaidi ya kumridhisha mwalimu na mzazi wake kwamba, kama watoto wengine, na yeye anao uwezo wa kukusanya na kukumbuka maarifa.Mazoea haya yanaibua changamoto kadhaa kimalezi kwa watoto.

Kulea tabia ya ushindani

Shule zetu zinathamini wanafunzi wanaofanya vizuri na kudhihaki wale wanaoonekana dhaifu. Mtoto anayefanya vizuri darasani, kwa mfano, ndiye anayependwa na walimu, ndiye anakuwa maarufu, na ndiye anayepata zawadi ya kuwa bora kuliko wengine. Hili ni tatizo na nitaeleza kwa nini.

Kwa muda mrefu tuliamini kumzawadia mtoto mdogo aliyefanya vizuri kuliko wenzake ingekuwa si tu motisha kwake kuongeza jitihada za kufanya vizuri kwa mara mwingine tena, lakini pia ingewafanya watoto wengine kuweka bidii zaidi kwa matarajio ya kupata zawadi kama aliyopewa mwenzao.

Hata hivyo, tafiti nyingi, mfano za Prof. Carol Dweck wa Chuo Kikuu cha Stanford, zinaonyesha utamaduni huu wa kuwapongeza watoto kwa namna inayobagua uwezo wao una kasoro nyingi zinazoweza kukuza mitazamo mibovu kwa watoto.  

Kwa mfano, mtoto aliyezoea kuongoza darasani na kusifiwa anaweza kugeuka kuwa mtumwa wa sifa. Utumwa huu wa sifa unamweka kwenye hatari ya kuwa na tabia ya kuelekeza nguvu kwenye eneo linalomfanya ajione bora na hivyo kukwepa maeneo mengine ambayo, pengine, yanaweza kuwa muhimu katika maisha.

Ikiwa, mathalani, mtoto anajua walimu na wazazi humsifia kwa kufaulu vizuri, mtoto huyu anaweza kukwepa  kushiriki kazi za ndani ambazo anajua haziwezi kumgusa mzazi wake.

Pia, kupongezwa kwa kuwazidi wengine kunaweza kumkatisha tamaa mtoto hasa pale inapotokea ama anafanya vizuri lakini hakuna mtu anayejali au basi kuna mtoto mwingine anayeonekana kumzidi kinyume na vile alivyozoea.

Lakini vile vile, kwa upande wa watoto wanaoshuhudia mwenzao akizawadiwa kwa kuwazidi mara kwa mara, wengi wao hunyong’onyea na kuanza kujiona kama watu duni wasio na uwezo wa kufanya vizuri kama wenzao.

Tafsiri yake ni kwamba, kwa watoto wadogo, hakuna sababu ya msingi ya kuwawekea mazingira ya kuwashindanisha kiuwezo hali inayoweza kuwaingizia dhana ya kushindana hata katika mazingira ambayo hakuna sababu yoyote ya ushindani.

Kudumaza vipaji

Changamoto ya pili ya shinikizo hili kubwa la taaluma kwa watoto, ni kudumaza vipaji ambavyo kimsingi hakuna namna ya kuvipima kwa kutumia mitihani. Kwa kuwa shughuli karibu zote zinazoendelea darasani zinalenga kujenga eneo moja tu la kukusanya na kukumbuka maarifa, mtoto hawezi kuwa na motisha ya kufanya vitu vingine visivyohusiana na masomo.

Matokeo yake mtoto anapokuwa shuleni anakuwa hana kazi nyingine zaidi ya kusoma, kuandika na kuhesabu. Anaporudi nyumbani, hali kadhalika, anakutana na mzazi anayeamini kazi ya msingi ya kufanya kwa mwanae ni kuzingatia masomo.

Mtoto anayeishi kwenye shinikizo la namna hii anapojaribu ‘kuchepuka’ kidogo ili kukuza vipaji visivyotambuliwa na mitihani rasmi ya darasani, anajikuta kwenye mgogoro na mwalimu na mzazi.

Kwa sababu hii, watoto wetu wengi ambao pengine wangeweza kuwa na vipaji vya kila aina, wanaishia kufanya vitu ambavyo mara nyingine haviwafanani.

Kudumaza ukuaji

Shinikizo hili kubwa la kufaulu masomo pia linaathiri mtindo wa kawaida wa maisha ya mtoto. Shule inayotaka mtoto awe bora kitaaluma, kwa mfano, kwa kawaida, itamnyima fursa ya kushiriki shughuli zisizo na kimasomo lakini ambazo kimsingi zingeweza kuwa muhimu kimakuzi.

Mtoto huyu mdogo shauri ya kusoma kwenye shule inayotaka kuongoza kwenye mitihani, hatopata mtu wa kumfundisha kujifanyia usafi wake binafsi, kufagia, kushiriki kazi za mikono kwa sababu tu mitihani ambayo ndio kipimo cha ubora wa shule haina vipengele vinavyopima utu wa mtoto, ushiriki wake kwenye kazi za mikono.

Pamoja na uzuri wa kufaulu masomo, mtoto mdogo wa shule ya msingi, kwa kweli, anahitaji kufaulu pia hata kwenye maeneo mengine yenye nafasi muhimu ya kumsaidia kupata mafanikio katika maisha.

Mbali na kupata alama 95 darasani, kwa mfano, mtoto huyu anahitaji kujifunza umuhimu wa kujali hisia na mahitaji ya wengine, tabia ambayo angeweza kujifunza vizuri zaidi kupitia michezo kuliko vitabu vilivyotajwa kwenye mtalaa.

Kasoro hii ya mfumo wa elimu kutilia mkazo eneo la ufahamu na maarifa kuliko maeneo mengine, imefanya watoto wengi wakose fursa pana ya kujengwa kiroho, kimaadili na hata kupata stadi nyingine muhimu za kimaisha.

Ushauri

Natambua shauku kubwa waliyanayo wazazi kuona watoto wanashika nafasi ya kwanza darasani. Hata hivyo, kama tulivyoona kwa ufupi, shauku hiyo ya kuwa na watoto wenye ‘akili’ isiwafanye watoto wakajikuta wakibanwa mno na hivyo kukosa muda wa kujifunza stadi nyingine za maisha.

Aidha, tunazo sababu za kutosha kuvumilia hata pale tunapoona watoto wetu hawafanyi vizuri darasani. Hakuna ushahidi wa kitafiti unaothibitisha kuwa ufaulu wa sekondari na vyuoni unategemea na ufaulu mkubwa wa ngazi za chini.

Miaka ya awali ina umuhimu mkubwa katika kujenga sura ya maisha atakayoishi mtoto. Tunahitaji kuweka msisitizo mkubwa kwenye kujenga utu, kuwakuza kiroho na kuwafundisha stadi za maisha, kwa sababu hayo ndiyo maeneo yatakayoamua mustakabali wao.


Pia, utamaduni wa kuwashindanisha watoto wa ngazi za chini hauna tija. Tunaweza kuwafanya watoto wakajifunza vizuri bila kuwaambia wameshika nafasi ya ngapi darasani. 

Mbinu za kukuza uwezo wa akili wa mtoto.



Kwa muda mrefu wataalam wengi wa saikolojia ya elimu waliamini uwezo wa akili anaokuwa nao mtu unarithiwa na haubadiliki. Katika kuthibitisha kuwa akili za mtu haziwezi kubadilika, wapo wataalam, tena wengi tu, waliobuni kipimo cha akili za mtu kilichojulikana kama IQ. Kipimo hiki kilitumia mfululizo wa maswali anayoulizwa mtu kujua anawezaje kufikiri, kuelewa na kuchambua mambo.

Lakini kadri utaalam wa kupima utendaji wa ubongo ulivyoendelea kuongezeka, sasa tunaelewa akili za binadamu zinaweza kubadilishwa na mazingira anayokutana nayo mtu.

Mtazamo huu mpya unatupa faida mbili kubwa. Kwanza, unatusaidia kujua mambo yanayoweza kufanyika kubadili uwezo wa akili anazokuwa nazo mtu. Pili, unaongeza wajibu tulionao sisi kama wazazi katika kumwekea mtoto mazingira sahihi yanayoweza kusisimua utendaji wa ubongo wake.

Katika makala haya tutazame mambo manne unayoweza kuyafanya kukuza uwezo wa mtoto kufikiri, kuelewa na kuhambua mambo.

Badili lugha anayojisemea mtoto

Kila mtu anayo lugha ya ndani anayoitumia kufikiri. Lugha hii ya ndani ina kazi kubwa ya kujenga vile unavyojichukulia. Unapofikiri jambo, kwa mfano, unaweza kusema maneno fulani yanayokuhamasisha, kukusifu, kukukosoa, kukutia wasiwasi, mashaka na hata kukukatisha tamaa.

Wataalam wanasema kuna uhusiano mkubwa kati ya mawazo ya mtu na kile anachokifanya. Kama mtoto, kwa mfano, atayaamini mawazo yanayomvunja moyo, matokeo yake yatakuwa ni kushindwa. Mtoto mwenye mawazo yanayomnyong’onyeza hawezi kuzidi mawazo hayo. Kukata tamaa, kujizomea, kujikosea kulikopitiliza, kunamnyima fursa ya kufikiri sawa sawa.

Mzazi jenga mazoea ya kumsemea mwanao maneno yanayomjenga. Tambua mazuri anayoyafanya na yaseme maneno chanya. Usiwe na tabia ya kumkosoa mno mtoto hata kama kweli hajafanya vizuri.

Fikiria mtoto amefanya vibaya darasani. Mzazi wa kwanza anamwambia, “Nikijua tu utafeli. Kwanza huna akili. Naona napoteza tu hela kukusomesha.”

Mzazi wa pili anamwambia, “Kwa namna ninavyokufahamu, uwezo wako ni mkubwa. Najua ukikazana, ukimsikiliza mwalimu na kujisomea, uwezo wa kufanya bidii kufikia uwezo wako halisi.”

Mzazi wa kwanza anaongea kwa hasira shauri ya matajiro makubwa aliyonayo kwa mwanae. Hachagui maneno ya kumwambia mwanae kwa sababu anaamini kufeli mtihani ni kukosa akili. Hajua athari ya maneno yake katika kujenga lugha ya ndani itakayoathiri uwezo wake wa kujituma.

Mzazi wa pili anaweza kuwa na hasira lakini anajua nguvu ya maneno yake. Anamtamkia mtoto maneno yanayomtia hamasa hata katika kufeli kwake. Maneno haya chanya yatajenga lugha chanya itakayokuwa hamasa ya kufanya vizuri zaidi.

Ongeza fursa za mawasiliano

Mazungumzo yana nafasi kubwa ya kuongeza uwezo wa akili anaokuwa nao mtu. Kuzungumza na mwanao mara kwa mara kunakuza uwezo wake wa lugha, msamiati wake, na hata kusisimua utendaji wa ubongo wake.

Unaweza kushangaa lakini ndivyo wataalam wanavyotuambia. Wazazi waongeaji wenye tabia ya kuzungumza na watoto huwasaidia kuwa na msamiati zaidi.

Lugha ina nafasi kubwa katika kujenga uwezo wa akili.

Bila kujali umri wake, jenga mazoea ya kujadiliana na wanao masuala mbalimbali yanayohusu maisha yao. Wape nafasi ya kukusimulia yale wanayokutana nayo shuleni, kwenye michezo, mambo wanayoyasikia mitaani, matarajio waliyonayo na hata hofu wanazohitaji kupambana nazo. Fanya mazungumzo yawe utaratibu wa kawaida wa maisha ya hapo nyumbani.

Mfano, mwombe mwanao akuambie siku yake imekwendaje. Mwuulize maswali yanayomtaka ajieleze badala ya kujibu kirahisi ‘ndiyo’, ‘hapana’ na ‘sijui.’ Mruhusu mtoto akuulize maswali na jitahidi kuyajibu kadri unavyoweza.

Mara nyingi mtoto huuliza kutaka kuyaelewa mazingira yake, kuelewa mambo anayoyaona na kukutana nayo katika maisha. Kumbuka muhimu hapa sio majibu unayompa, bali uwezo wa kufikiri, kuelewa, na kuchambua mambo anayoyasikia.

Simulia hadithi

Tangu zamani utamaduni wetu ulitambua umuhimu wa masimulizi kwa watoto. Nyakati za jioni, wazazi walikuwa na utaratibu wa kukaa na watoto wao na kuwasimulia hadithi mbalimbali.

Hadithi hizi, mbali na kukuza ukaribu baina ya wazazi na watoto wao, zilikuza uwezo wa watoto kufikiri. Hadithi, mathalani, zinatumia wahusika wenye tabia na mikakati tofauti kwa kutumia madhari ya kufikirika. Haya yote humfanya mtoto alinganisha anayoyasikia na maisha yake ya kila siku.

Siku hizi desturi hii, hata hivyo, imeanza kupungua. Watoto wanatumia muda mwingi kufanya kazi za kitaaluma ambazo mara nyingine hazihusiani na maisha yao ya kila siku. Mbali na kufifiisha uwezo wao wa kuyaelewa mazingira yao, kazi hizi nyingi zinafunga fikra zao kwenye mambo fulani pekee.

Tunahitaji kufufua desturi ya hadithi kwa watoto. Mbali na kuwasimulia, tuwape nafasi wao wenyewe wabuni hadithi kuwasaidia kujua kuchagua wahusika, kupangilia matukio na kusema wanachokifikiri.

Hamasisha usomaji wa vitabu

Sambamba na masimulizi, mzazi una fursa ya kumhamasisha mtoto kusoma vitabu. Unaweza kuanza kwa kumsomea kitabu chenye hadithi zinazogusa mambo anayokutana nayo kwenye maisha.

Usomaji wa vitabu kwa watoto si tu unaimarisha uhusiano wenu, lakini unaongeza kumbukumbu, uzingativu na hata kukuza msamiati.

Hata hivyo, ni muhimu kuzingatia kuwa huwezi kukuza tabia fulani kwa mtoto kama wewe mwenyewe huna. Lazima kwanza uanze wewe mwenyewe kupenda kusoma ili mwanao ajifunze.

Swali kwako mzazi, kwa mwaka 2017 ulisoma vitabu vingapi? Je, uliwahi kuonekana ukisoma hapo nyumbani au muda mwingi unautumia kutazama televisheni na kutumia simu?

Je, kuna vitabu vinaonekana kwenye mazingira ya nyumbani?

Lenga kumfundisha mwanao kwa vitendo. Onekana ukisoma ukiwa nyumbani. Kama huna vitabu au magazeti, unavyo vitabu vya dini. Anza na hivyo.

Pia, mnunulie vitabu kama zawadi yake na msomee nyakati za jioni anapojiandaa kulala. Watoto wanapenda sana fursa kama hizi. Kila inapowezekana, mpeleke kwenye maduka ya vitabu na maktaba kupanda mbegu ya mtoto kuwa na urafiki wa kudumu na maandishi.

Blogu: http://bwaya.blogspot.com

Sunday, December 17, 2017

Kumlea mtoto bila viboko inawezekana.

Malezi bora huhitaji msingi imara kama ilivyo kwa ujenzi wa nyumba. Leo tunaangazia swala la viboko katika malezi na kujielimisha kama inawezekana kulea bila viboko. Haishangazi kuwaona wazazi katika jamii yetu wakichapa fimbo, kwenzi, kumkaripia kwa sauti ya juu (kufoka) na hata kumtusi mtoto wao. Tofauti na dhana iliyojengeka kuwa namna hii mtoto anapata kujifunza utii, watalaamu wa makuzi wanatwambia kuwa mtoto anaweza kutii bila viboko. Hii inajulikana kama uadabishaji chanya unaojengwa kupitia mahusiano mazuri baina ya mtoto na mlezi wake.

Zifuatazo ni nyenzo kuu nne za kujenga msingi bora wa malezi yenye uadabishaji chanya na ambayo hufikia malengo endelevu ya mzazi kwa mtoto wake.

Kuwa na malengo ya muda mrefu juu ya mtoto wako. Kufanikisha kumkuza mtoto tangu anapozaliwa hadi utu-uzima ni kazi ya kujivunia, lakini wazazi wengi huianza safari hii bila kufikiria ni upi mwisho wa safari hii? Ukifanikiwa kujua malengo ya muda mrefu kwa mtoto wako, wewe mwenyewe utakuwa mfano wa kuigwa. Kama unataka mtoto wako awe mwema na mwenye msaada kwa jamii, anayeweza kufikiri, msikivu, asiye mkorofi, mwenye upendo kwa watu wote na mengine kama hayo lazima utembee katika nyayo hizo. Akuige. Ukipanda mahindi huvuni viazi.

Mtengenzee mtoto mazingira ya upendo na mawasiliano. Upendo na mawasiliano kati ya mzazi na mtoto kwa jamii yetu huishia mara nyingi umri wa kuhudhuria kliniki (miaka5). Ili kumkuza mtoto mwema unatakiwa kumuonyesha upendo wakati wote na kumpatia taarifa muhimu hasa kuhusu mabadiliko ya kimwili pale anapoelekea balehe, mfanye mtoto awe rafiki na kwamba kuwa mzazi sio lazima mtoto akuogope bali akuheshimu na kukuthamini.

Elewa watoto wanavyofikiri na kuhisi juu ya mambo mbalimbali. Jipe muda kuelewa hisia na fikra za watoto juu ya mambo mbalimbali kulingana na umri wao. Utakuta mzazi anampiga mtoto mchanga/mdogo kisa analia pasi kikomo usiku na mchana bila ya kujiuliza iwapo mtoto anaelewa hata sababu ya kupigwa? Yapo makosa mengi watoto wanayofanya katika umri tofauti na wazazi hutumia vipigo kama namna ya kuwaadabisha bila ya kujua sababu za watoto (kiumri) kufanya wafanyayo. Vipigo namna hii vinawatengenezea tabia ya kuwa wakorofi na kuamini kuwa matatizo hutatuliwa kwa njia ya ugomvi. Usugu!

Adhabu ni malengo ya muda mfupi. Uelewa juu ya changamoto mbalimbali zitokanazo na hatua za makuzi ya mtoto na namna ya kuzikabili kwa kutumia mbinu rafiki na si viboko ni muhimu kwa mzazi. Utakubaliana nasi kuwa viboko vinamneemesha mzazi/mlezi zaidi hata ya mtoto kwani anapata kutuliza hasira zake huku mtoto akiambulia mafunzo hafifu mno. Kutumia adhabu katika kumuadabisha mtoto hutimiza malengo ya muda mfupi na hulenga katika kutimiza matakwa ya mzazi ya muda huo na si malengo endelevu.

Adhabu za viboko na nyinginezo hugusa zaidi mwili tu na husahaulika kwa muda mfupi wakati kuadabisha kwa njia rafiki hugusa ubongo moja kwa moja na humpa mtoto nafasi ya kufikiri na kujifunza kutokana na makosa. Malezi yanayolenga kukuza mtoto ambaye mzazi anategemea aje kuwa mtu mzima muwajibikaji na anayekubalika kwenye jamii hayana budi kuzingatia nyenzo hizi.

Mambo matano unayoyahitaji ili uishi vizuri na watu kazini.


Sehemu kubwa ya maisha ya kazi hutegemea vile unavyoweza kukaa na watu bila migongano.

Unapofanya kazi na watu msioelewana, unajiweka kwenye mazingira yanayoweza kukupunguzia si tu ari ya kufanya kazi, bali hata ufanisi wako.

Kama ilivyo mitaani tunakoishi, wapo watu kazini huwezi kuwaridhisha. Unaweza kufanya kila lililo kwenye uwezo wako, lakini bado wakaendelea kukuchukia.

Hata hivyo, ni vizuri kuelewa kuwa si mara zote watu hujenga chuki na wewe kwa sababu tu hawakupendi. Wakati mwingine, tabia ulizonazo (bila wewe kujua) zinaweza kuchochea hisia za wivu, uadui na hata mashindano yanayoweza kuathiri mahusiano yako na watu.

Katika makala haya, tunajifunza tabia tano zitakazokusaidia kuwa na uhusiano mzuri na wafanyakazi wenzako.

Kuwa tayari kuzidiwa

Katika mazingira ya kazi hisia za kuzidiana hazikosekani. Watu huweza kushindana kimyakimya kwa viwango vya elimu; uzoefu; utendaji wa kazi; ushawishi na hata tija waliyoileta kwa kampuni.

Usipokuwa makini unaweza kuingia kwenye mtego wa mashindano haya yanayoweza kuwa chanzo cha misuguano na wafanyakazi wenzako.

Mtu anayeona fahari kushindana na wenzake, mathalani, anaweza kuwa mtu wa kuzungumza sana kwenye vikao. Atashauri mahali ambako ushauri wake haujaombwa ilmradi tu aonekane ni mjuzi wa mambo.

Lakini pia, kwa kuwa anataka kuonekana anawazidi wengine hatakuwa tayari kujifunza kwa wenzake. Haya yote yatamtengenezea ufa wa uhusiano kati yake na wenzake.

Unahitaji kujifunza kuwa mnyenyekevu hata kama kweli inawezekana unawazidi watu. Jijengee mazingira ya kuomba msaada kwa watu wanaokuzidi uzoefu na ujuzi. Fanya hivyo kwa uangalifu bila kuwafanya watu wawe na wasiwasi na uwezo wako.

Sambamba na hilo, usiwe mwepesi wa kushauri kama ushauri wako haujahitajika. Badala yake jenga weledi utakaowafanya watu wakufuate wenyewe kwa ushauri.

Ukiweza kufanya hivyo, watu watakuchukulia kama rafiki asiye mshindani. Utajipunguzia maadui na mapambano yasiyo ya lazima.

Tatua changamoto za wengine

Kila mtu kazini huwa na malengo yake. Inawezekana, kwa mfano, kwa nafasi yako, ukawa na malengo ya kuongeza uzalishaji wa kampuni. Haya ni malengo ya kitaasisi.

Lakini pia unaweza kuwa na malengo yako binafsi kama kupanda cheo. Si jambo baya kuwa na malengo yako kama mfanyakazi anayejitambua.

Unapofanya hivyo, ni vizuri kuelewa kuwa kila mfanyakazi naye ana malengo yake.

Wakati mwingine malengo yako yanaweza kuingilia na malengo ya mwingine.

Ukitaka kukaa na watu vizuri, jifunze kuongeza thamani yako kwa kufikiria namna unavyoweza kuwasaidia wenzako kufikia malengo yao.

Jambo la kukumbuka ni kuwasaidia wengine kufikia malengo yao, unaweza kujikuta wakati mwingine watu hao wanapata sifa kupitia mgongo wako.

Huna sababu ya kuumia wala kujiona umetumika.

Watu hao mbali na kuwawekea mazingira ya kukulipa fadhila siku nyingine utakapowahitaji, hawatakuwa na sababu ya kushindana na wewe.

Jifunze kuanzia chini

Kwa kawaida watu wanaoanza kazi huwa na matarajio makubwa. Inawezekana ni ndoto za kulipwa mishahara minono itakayobadilisha maisha yako ndani ya muda mfupi.

Ukiacha kipato, kuna mambo ya vyeo. Wafanyakazi wapya hufikiri ni rahisi kukwea ngazi na kupewa madaraka makubwa.

Fikra kuwa unaweza kuanzia juu haraka zinaweza kukuingiza kwenye matatizo yasiyo ya lazima. Kwanza, utakosa uvumilivu wa kufanya kazi chini ya watu wengine kwa kujiona una sifa za kutosha kukupandisha juu kimamlaka. Lakini pia tabia yako inaweza kuonesha papara na kiburi kisicho na sababu.

Unahitaji kuwa mtu wa subira

Jizuie kujipatia sifa za harakaharaka. Ukweli ni kwamba, mafanikio yoyote kazini ni matokeo ya jitihada na bidii zinazoweza kuchukua muda kulipa. Kila aliyefanikiwa leo alianza chini. Ili ufanikiwe unahitaji kuwa na subira.

Kuwa mwaminifu kwa wenzako

Mazingira ya kazi hayakosi watu wanaopenda kueneza habari mbaya. Utakaa na mtu unayemheshimu wakati wa chai kisha ataanzisha mazungumzo yanayomhusu mtu asiyekuwepo kwenye mazungumzo hayo.

Mara nyingi mazungumzo haya huwa na lengo la kuwabomoa wengine. Tabia hii wakati mwingine hulenga kuimarisha makundi ya kimaslahi kazini.

Kwa kawaida, majungu ni kazi ya watu wasio na kazi; watu wasiojiamini au watu wanaolinda maslahi binafsi kwa kubomoa heshima za wengine. Jambo la kuzingatia ni kuwa hao hao unaopiga nao majungu hukosa imani na wewe.

Jenga utaratibu wa kulinda heshima ya wenzako hata wanapokuwa hawapo kwenye mazungumzo.

Unaposikia habari mbaya za mfanyakazi mwenzako, usiwe mwepesi kushabikia. Habari mbaya zilizobomoa heshima ya mwenzako hazikusaidii kuongeza ufanisi wako.

Badala ya kushabikia mazungumzo yanayomharibia mwenzako asiyekuwepo, tafuta jambo jema na liseme kwa ujasiri. Watu wakikufahamu kwa tabia hiyo ya kukwepa kuwa sehemu ya makundi yanayofuga ‘siasa’ za maslahi kazini, utajenga kuaminika kazini. Mbinu chafu zinaposukwa dhidi yako, utakuwa na watu watakaokuwa tayari kukutetea.

Kubali kukosewa na watu

Unajisikiaje unapogundua mtu uliyemheshimu anasuka mpango wa kukuchafua na kukuharibia heshima yako? Je, utafikiria kulipa kisasi au kuachana naye na kuendelea na hamsini zako?

Ofisi hukutanisha watu wenye mawazo na hulka tofauti. Unaweza kujitahidi kuishi vizuri na watu, lakini bado wakawapo watu watakaochukulia wema huo kama sababu ya kukosana na wewe.

Hali hii isikuvunje moyo. Jichukulie kama binadamu anayeweza kuchukiwa bila sababu na mtu yeyote.

Jichukulie kama mtu anayeweza kufanyiwa visa na watu wenye kutumia mbinu chafu kufikia malengo yao. Ukielewa hivyo, hutapata shida unapogundua kuna watu wanakuzunguka.

Kufanya hivyo, hata hivyo, haimaanishi kukubali kuonewa bila sababu.

Hapana. Jenga ukomavu wa kufanya kazi na watu wasiokupenda bila kuathiri kazi zako.

Christian Bwaya ni Mhadhiri wa Saikolojia, Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge (MWECAU), Moshi. http://bwaya.blogspot.com , 0754 870 815

Friday, October 27, 2017

Maumbo ya wanawake wakimbizi yabomoa ndoa za watu Kigoma

Maumbo ya wanawake wakimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi huko mkoani Kigoma yamezua gumzo baada ya akina Baba kuzitelekeza familia zao na kuoa wanawake hao wakirundi.

Baadhi ya Wanaume katika wilaya ya Kakonko wanadaiwa kutelekeza ndoa zao na kwenda kuoa wanawake hao wa Kirundi huku sababu ikiwa ni uzuri maumbo yao.

Hayo yameelezwa na wanawake wa kijiji cha Kaziramihunda, kilichopo kata ya Kasanda wilayani Kakonko mkoani Kigoma mbele ya Mkuu wa wilaya hiyo, Kanali Hosea Ndagala.

Akizungumza kwa niaba ya wanawake wa kijiji hicho Bi. Tabu Kiuliko amesema anamuomba Mkuu wa Wilaya kuingilia kati suala hilo la kutelekezwa na wanaume zao kwani limekuwa sugu na limerudisha nyuma maendeleo ya baadhi ya familia.

“Wanawake wengi wameachiwa jukumu la ulezi wa familia baada ya waume zao kuwatelekeza wake zao na kuoa wakimbizi , tunaomba serikali iingilie kati suala hilo,“amesema Bi. Tabu.

Hata hivyo, Afisa Mtendaji wa kata ya Kasanda, Motoni Borutu ameunga mkono taarifa hiyo kwa kukiri kuwa Ofisi yake imepokea malalamiko hayo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Kwa upande mwingine, Afisa Uhamiaji wa wilaya ya Kakonko, Christopher Mlemeta ambaye alikuwa kwenye msafara huo wa mkuu wa wilaya, amesema ni kosa kisheria kwa mtu kuoa au kuolewa na mkimbizi na kuishi naye nchini bila kupata kibali maalumu kutoka serikalini.

Chanzo:Mwananchi