Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

HABARI KWA WAKATI KUTOKA HAPA

Tunakuhakikishia kupata habari zote zilizo muhimu kutoka ulimwenguni kote kwa wakati, unaweza kusubscribe mtandao wetu na ukawa unapokea habari zote katika email yako punde tu tuchapishapo machapisho yetu. Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

Labels

Showing posts with label MAHUSIANO. Show all posts
Showing posts with label MAHUSIANO. Show all posts

Monday, March 19, 2018

Jinsi ya kufanya ili mtoto apende chakula.

Wazazi wengi hasa waishio mijini wanakumbana na changamoto ya watoto wao kutopenda kula ama kwa kukosa hamu na hata vinginevyo. Tumepata wasaa wa kuzungumza na mtaalamu wa lishe kutoka Shirika la Chakula Dunia (WFP), Neema Shosho na hapa tutakupa machache juu ya nini ufanye mwanao apende kula.Shosho anashauri kwamba wakati wa kumlisha mtoto ni vyema mzazi au mlezi utumie lugha ya upole na upendo ili kumuhamasisha mtoto kula. Lugha za matusi, vitisho...

Alama 11 za mpenzi mwenye mchepuko.

Kila mmoja atakubaliana na mimi kwamba uhusiano baina ya wapendanao ulikusudiwa kuwa ya upendo, maelewano, kuaminiana na urafiki wa hali ya juu. Kwa bahati mbaya hali halisi siyo hiyo katika mahusiano ya wengi. Wengi wetu wameumizwa kwa mpenzi mmoja au mara nyingine wote kutokuwa waaminifu katika mahusiano yao.Kutokuwa mwaminifu hapa namaanisha hali ya mpenzi mmoja kuwa na mahusiano yasiyo rasmi na mpenzi au wapenzi wengine pembeni au mchepuko...

Tuesday, January 9, 2018

Umuhimu wa Kumpunguzia Mtoto Shinikizo la Kufaulu

Ufaulu wa mitihani umepewa nafasi ya pekee katika mfumo wetu wa elimu. Shule zetu, kwa hakika, hazina namna nyingine ya kumwelimisha mtoto zaidi ya kumtaka akusanye, akumbuke na kutumia maarifa aliyonayo kujibu maswali ya mtihani. Ingawa ustawi wa jumla wa mwanadamu hautegemei eneo hilo moja la ukusanyaji na utumiaji wa maarifa, shule zetu zinaonekana kuamini pasipo mtu kuwa na maarifa mengi hawezi kufanikiwa. Kasumba hii imetuathiri...

Mbinu za kukuza uwezo wa akili wa mtoto.

Kwa muda mrefu wataalam wengi wa saikolojia ya elimu waliamini uwezo wa akili anaokuwa nao mtu unarithiwa na haubadiliki. Katika kuthibitisha kuwa akili za mtu haziwezi kubadilika, wapo wataalam, tena wengi tu, waliobuni kipimo cha akili za mtu kilichojulikana kama IQ. Kipimo hiki kilitumia mfululizo wa maswali anayoulizwa mtu kujua anawezaje kufikiri, kuelewa na kuchambua mambo. Lakini kadri utaalam wa kupima utendaji wa ubongo ulivyoendelea...

Sunday, December 17, 2017

Kumlea mtoto bila viboko inawezekana.

Malezi bora huhitaji msingi imara kama ilivyo kwa ujenzi wa nyumba. Leo tunaangazia swala la viboko katika malezi na kujielimisha kama inawezekana kulea bila viboko. Haishangazi kuwaona wazazi katika jamii yetu wakichapa fimbo, kwenzi, kumkaripia kwa sauti ya juu (kufoka) na hata kumtusi mtoto wao. Tofauti na dhana iliyojengeka kuwa namna hii mtoto anapata kujifunza utii, watalaamu wa makuzi wanatwambia kuwa mtoto anaweza kutii bila viboko. Hii...

Mambo matano unayoyahitaji ili uishi vizuri na watu kazini.

Sehemu kubwa ya maisha ya kazi hutegemea vile unavyoweza kukaa na watu bila migongano. Unapofanya kazi na watu msioelewana, unajiweka kwenye mazingira yanayoweza kukupunguzia si tu ari ya kufanya kazi, bali hata ufanisi wako. Kama ilivyo mitaani tunakoishi, wapo watu kazini huwezi kuwaridhisha. Unaweza kufanya kila lililo kwenye uwezo wako, lakini bado wakaendelea kukuchukia. Hata hivyo, ni vizuri kuelewa kuwa si mara zote watu hujenga chuki...

Friday, October 27, 2017

Maumbo ya wanawake wakimbizi yabomoa ndoa za watu Kigoma

Maumbo ya wanawake wakimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi huko mkoani Kigoma yamezua gumzo baada ya akina Baba kuzitelekeza familia zao na kuoa wanawake hao wakirundi.Baadhi ya Wanaume katika wilaya ya Kakonko wanadaiwa kutelekeza ndoa zao na kwenda kuoa wanawake hao wa Kirundi huku sababu ikiwa ni uzuri maumbo yao.Hayo yameelezwa na wanawake wa kijiji cha Kaziramihunda, kilichopo kata ya Kasanda wilayani Kakonko mkoani Kigoma mbele ya Mkuu wa...