Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais
TAMISEMI Mohamed Pawaga, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa kwanza
wa Maafisa Lishe wa Mikoa nchini ambao unahusisha Wataalam wa kada hiyo
waliopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii
na Lishe ambao wenye lengo la kuboresha lishe katika Jamii. Mkutano huo
unafanyika katika Chuo cha Mipango mjini Dodoma. Kulia kwake ni Stephen
Motambi Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI
na kushoto kwake ni Dkt. Rasheed MAftah ambaye ni Mkurugenzi wa Afya,
Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI
Stephen Motambi Mkurugenzi
Msaidizi wa Huduma za Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI akitoa neno la
utangulizi wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Maafisa Lishe wa
Mikoa nchini ambao unahusisha Wataalam wa kada hiyo waliopo chini ya
Ofisi ya Rais TAMISEMI, Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe ambao
wenye lengo la kuboresha lishe katika Jamii
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa
kwanza wa Maafisa Lishe wa Mikoa nchini ambao unahusisha Wataalam wa
kada hiyo waliopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Idara ya Afya, Ustawi
wa Jamii na Lishe ambao wenye lengo la kuboresha lishe katika Jamii,
wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika
kikao kazi cha kwanza cha Maafisa Lishe wa Mikoa nchini ambao unahusisha
Wataalam wa kada hiyo waliopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Idara ya
Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe ambao wenye lengo la kuboresha lishe
katika Jamii, wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi. Mkutano
uliofanyika katika chuo cha Mipango Dodoma
…………….
Kaimu Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais TAMISEMI Mohamed Pawaga, amefungua mkutano wa kwanza wa
Maafisa Lishe wa Mikoa nchini ambao unahusisha Wataalam wa kada hiyo
waliopo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii
na Lishe ambao una lengo la kuboresha lishe katika Jamii.
Akifungua kikao hicho
mjini Dodoma, Kaimu Katibu Mkuu Mohamed Pawaga, amesema tatizo la
utapiamlo kwa watoto walio chini ya miaka mitano nchini limepungua kwa
kiasi kikubwa. “takwimu za Utafiti wa Afya na Demografia Nchini za mwaka
2015/16 zimebaini kupungua kwa viwango vya Kitaifa vya utapiamlo hasa
kwa watoto chini ya umri wa miaka 5 kwa viashiria vya Udumavu, Ukondefu
na Uzito pungufu ukilinganisha na hali ilivyokuwa mwaka 2010.
Aidha amesema,
kiwango cha Udumavu Kitaifa kimepungua kutoka asilimia 42.8 hadi 34.7,
Ukondefu kutoka asilimia 4.8 hadi 3.0 na Uzito Pungufu kutoka asilimia
16 hadi 13, jambo ambalo amesema ni jitihada kati ya Serikali na Wadau
katika masuala ya lishe.
Amewataka washiriki
hao kufanya kazi stahili na kutoa taarifa za kila robo ya mwaka wa fedha
kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ili wafahamu kuhusu
maendeleo ya utekelezaji wa shughuli za Lishe kulingana na Mkataba
watakaosaini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI mwishoni mwa
mwezi Desemba, 2017.
Amewataka washiriki
kuufanyia kazi Mpango Jumuishi wa Lishe wa Taifa – 2016/2021 ambao
umejikita kwenye maeneo matatu ya Mpango wa pamoja, Usimamizi wa pamoja
na Uratibu wa pamoja wa shughuli za Lishe kati ya Serikali na wadau
lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa uwajibikaji, uwazi na ufanisi unakuwepo
ili kujitathmini ni eneo lipi linafanywa vizuri na lipi linahitaji
kuboreshwa ili kupunguza utapiamlo katika jamii.
Kwa upande wake Dkt.
Rasheed MAftah ambaye ni Mkurugenzi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma
za Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI, amesema kuwa, Mkutano wa kazi huo una
lengo la kujadili mbinu za utendaji kazi na kuwapa Maafisa Lishe
maelekezo muhimu kuhusu utendaji kazi ikiwa ni sehemu ya kuwajengea
uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuleta matokeo bora
katika kuimarisha hali ya Lishe nchini na hasa katika kutekeleza “Mpango
Jumuishi wa Lishe wa Taifa, 2016 – 2017”
Bwana Stephen Motambi
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema
kuwa kikao kazi hicho kina lengo la kuwajengea uwezo Maafisa Lishe wa
Mikoa ili kuweza kutekeleza shughuli za Lishe katika mikoa yao kwani kwa
hivi sasa nchini hali ya udumavu bado si nzuri sana mbayo ni watoto 34
kati ya 100 wanakabiliwa na utapiamlo unaotokana na lishe duni hivyo
Washiriki watajadili suala la lishe kama changamoto mojawapo ili
kupunguza idadi ya watoto wadumavu ambao wanaliongezea gharama Taifa kwa
matibabu yao.
Naye msoma risala ya
washiriki, Rehema Napegwa amesema ili kufanikisha utekelezaji wa Mpango
Jumuishi wa Taifa wa Lishe wa Julai 2015/16 hadi Juni 2020/21 na kuleta
matokeo yaliokusudiwa ni mapendekezo yetu kuboresha na kutatua
changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mkakati wa lishe wa
Taifa wa mwaka 2011/12 hadi 2015/16, ikiwa ni pamoja na kuongeze bajeti
yake katika kutekeleza afua za lishe na kutoa vibali vya ajira ili Mikoa
na Halmashauri ziweze kuajiri watalaamu wa lishe.
0 comments:
Post a Comment