Beki wa timu ya Simba SC Abdi
Banda ameaga rasmi jana baada ya timu yake kushinda Kombe la Shirikisho
kwa kuipiga bao 2 kwa moja Mbao FC katika mchezo uliofanyika mjini
Dodoma
Abdi Banda akiwa na wachezaji wengine wa Simba wakifurahia ubingwa wa Kombe la Shirikisho jana.
Abdi
Banda anasema imefika wakati sasa anapaswa kutafuta maisha mengine nje
ya klabu hiyo au sehemu nyingine huku akisema atakumbuka mambo mengi
mazuri katika klabu hiyo
"Ahsante Mungu nashukuru kwa
hiki ulichotujaalia. Zawadi ya mashabiki wa Simba nawaachia acha na
mimi nitafute maisha sehemu nyingine. Nitamiss vitu vingi hasa 'support'
yenu na moyo wenu wa uvumilivu ahsanteni sana na kwaherini" aliandika Abdi Banda
0 comments:
Post a Comment