Polisi katika mji wa Lagos nchini Nigeria wanasema kuwa
wanamchunguzua mwanamuziki Davido, ambaye jina lake kamili ni David
Adeleke, kufuatia utata unaozunguka kifo cha rafiki yake Tagbo Umeike.
Msemaji
wa polisi aliliambia shirika la utangazaji la Uingereza kuwa Davido hachukuliwa kuwa mshukiwa wakati
huu, lakini akathibitisha kuwa mwanamuziki huyo wa afrobeats, aliitwa
kuhojiwa pamoja na familia ya Tagbo, ambao walikuwepo wakati wa kifo
chake.
Tunachunguza ni wapi Davido alienda, kanda ya video, ili kupata picha wazi kuhusu kile kilichotokea. alisema msemaji huyo.
Bw. Tagbo, rafiki yake Davido alifariki tarehe 3 Oktoba na mwili wake ukaachwa nje ya hospitali mjini Lagos.
Davido amekana kabisa kuhusika kwenye kifo cha rafiki yake.
0 comments:
Post a Comment