Msanii wa muziki wa bongo fleva Aslay
Isihaka ambaye kwa sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Natamba'
amefunguka na kushukuru uongozi wake mpya kwa kufanikisha yeye kuweza
kupata ndinga mpya aina ya BMW.
"Alhamdulillah Asantee Mungu kwa hiki ulichonipa naishukuru management yangu Chambusso na Mxcarter, nakupenda Mama yangu kokote ulipo kila hatua dua 'new car' Umma unaongea" alindika Aslay kupitia mtandao wake wa Facebook.
Aslay Isihaka kwa mara ya kwanza kuanza kumiliki gari yake alizawadiwa na uongozi wake wa kwanza wa Yamoto Band chini ya Mkubwa Fella katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake mwaka 2015
0 comments:
Post a Comment