Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

Labels

Wednesday, November 1, 2017

Aslay avuta ndinga mpya itizame hapa.

Msanii wa muziki wa bongo fleva Aslay Isihaka ambaye kwa sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Natamba' amefunguka na kushukuru uongozi wake mpya kwa kufanikisha yeye kuweza kupata ndinga mpya aina ya BMW. 
Aslay ambaye ndani ya muda mfupi ameweza kuachia nyimbo zaidi ya 10 na ngoma hizo nyingi kufanya vizuri na kupokelewa vyema na wananchi jambo ambalo limeweza kufungua milango kwa msanii huyo kuweza kupata show nyingi na mafanikio mbalimbali. 

"Alhamdulillah Asantee Mungu kwa hiki ulichonipa naishukuru management yangu Chambusso na Mxcarter, nakupenda Mama yangu kokote ulipo kila hatua dua 'new car' Umma unaongea" alindika Aslay kupitia mtandao wake wa Facebook. 


Aslay Isihaka kwa mara ya kwanza kuanza kumiliki gari yake alizawadiwa na uongozi wake wa kwanza wa Yamoto Band chini ya Mkubwa Fella katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake mwaka 2015

0 comments:

Post a Comment