Mkataba mpya wa kimataifa wa kulinda haki za waandishi wa habari umetiwa saini huko Tunisia. 
Anthony Bellanger Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la 
Waandishi wa Habari (IFJ) amesema huko Tunisia kuwa  mktaba huo mpya 
umesainiwa kwa lengo la kuunda kamati itakayokuwa na jukumu la kudhamini
 usalama na kulinda maisha ya waandishi wa habari.
Bellanger ameongeza kuwa kamati hiyo 
itakayoundwa itakuwa na wajumbe 15 na wanachama wake watachaguliwa 
kutoka nchi zilizosaini kipengee cha 19 cha azimio la kimataifa la haki 
za kiraia na kisiasa ambacho kinabainisha wazi suala la kulindwa haki ya
 uhuru wa kifikra na kujieleza. 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa 
la Waandishi wa Habari (IFJ) amesema kuwa vitendo vya utumiaji mabavu 
dhidi ya waandishi wa habari duniani vinaongezeka kila uchao na uhalifu 
mwingi unaowakumba wana taaluma hao haufatiliwi na wahusika wa vitendo 
hivyo hawachukuliwi hatua za kisheria au kuadhibiwa.
Ni kwa sababu hiyo ndio maana Mkutano wa
 Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari umeratibu mpango mpya 
kwa ajili ya kuuungwa mkono kimataifa waandishi wa habari sambamba na 
kulindwa maisha yao wakati wa vita na amani ambao utawasilishwa katika 
kikao cha kawaida cha Umoja wa Mataifa. 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment