Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

Labels

Tuesday, November 21, 2017

Mkataba wa kimataifa wa kulinda haki za waandishi habari wasainiwa Tunisia.


    Mkataba wa kimataifa wa kulinda haki za waandishi habari wasainiwa Tunisia

Mkataba mpya wa kimataifa wa kulinda haki za waandishi wa habari umetiwa saini huko Tunisia.
Anthony Bellanger Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari (IFJ) amesema huko Tunisia kuwa  mktaba huo mpya umesainiwa kwa lengo la kuunda kamati itakayokuwa na jukumu la kudhamini usalama na kulinda maisha ya waandishi wa habari.
Bellanger ameongeza kuwa kamati hiyo itakayoundwa itakuwa na wajumbe 15 na wanachama wake watachaguliwa kutoka nchi zilizosaini kipengee cha 19 cha azimio la kimataifa la haki za kiraia na kisiasa ambacho kinabainisha wazi suala la kulindwa haki ya uhuru wa kifikra na kujieleza. 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari (IFJ) amesema kuwa vitendo vya utumiaji mabavu dhidi ya waandishi wa habari duniani vinaongezeka kila uchao na uhalifu mwingi unaowakumba wana taaluma hao haufatiliwi na wahusika wa vitendo hivyo hawachukuliwi hatua za kisheria au kuadhibiwa.

Mfano halisi wa mashambulizi dhidi ya waandishi habari 

Ni kwa sababu hiyo ndio maana Mkutano wa Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari umeratibu mpango mpya kwa ajili ya kuuungwa mkono kimataifa waandishi wa habari sambamba na kulindwa maisha yao wakati wa vita na amani ambao utawasilishwa katika kikao cha kawaida cha Umoja wa Mataifa. 

0 comments:

Post a Comment