Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

Labels

Tuesday, November 21, 2017

UNICEF: Watoto milioni 180 duniani, wakiwamo Watanzania hawana mustakabali mwema.

UNICEF: Watoto milioni 180 duniani, wakiwamo Watanzania hawana mustakabali mwema
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF limesema licha ya hatua zilizopigwa kimataifa, mtoto 1 kati ya 12 duniani wanaishi katika nchi ambazo matarajio yao leo ni mabaya kuliko ya wazazi wao.

Tathmini hiyo ya UNICEF imetolewa Jumatatu Novemba 20 kwa munasaba wa Siku ya Kimataifa ya Mtoto.

Ripoti ya UNICEF imesema watoto milioni 180 wanaishi katika nchi 37 ambako wanakabiliwa na ufukara, kutosoma au kuuawa kikatili kuliko watoto walioishi katika nchi hizo hizo miaka 20 iliyopita.

Mkurugenzi wa takwimu, utafiti na sera wa UNICEF Laurence Chandy anasema wakati kizazi kilichopita kimeshuhudia hatua kubwa katika kupandisha kiwango cha maisha ya watoto duniani, ukweli unasalia kwamba watoto kutoka jamii za walio wachache zilizosahaulika wametengwa katika hatua hizo na sio kosa lao wala la familia zao.
Watoto wanaolazimishwa kuhudumu kama askari vitani
Kwa mujibu wa tathimini hiyo idadi ya watu wanaoishi chini ya dola 1.90 kwa siku imeongezeka katika nchi 14, huku uandikishaji wa watoto wanaoingia shule za msingi ukishuka katika nchi 21 zikiwemo Syria na Tanzania, na vifo miongoni mwa watoto wa chini ya miaka 19 vikiongezeka katika nchi 7 zikijumuisha Sudan Kusini na Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR.

UNICEF inasema sababu kubwa ni, vita, ugaidi, matatizo ya kiuchumi, kuongezeka kwa idadi ya watu na umasikini.

0 comments:

Post a Comment