Tume ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza disemba 23 mwaka ujao kuwa ndio siku ya uchaguzi mkuu utakaojumuisha wa rais, wabunge na viongozi wa serikali za majimbo badala ya kufanyika mwaka 2019 kama ilivyokuwa imetangazwa hapo awali na Tume hiyo.
Kulingana na Chapisho hilo la ratiba ya Uchaguzi matokeo ya muda yatatangazwa katika kipindi cha wiki moja baada ya upigaji kura kufanyika, mnamo tarehe 30 Desemba, lakini matokeo kamili yatatangazwa tarehe 9 januari, 2019 na siku tatu baadae Rais Mteule Kuapishwa kushika hatamu.
Licha ya kurejesha Nyuma tarehe ya Uchaguzi Upinzani Nchini humo umeendelea kushikilia Msimamo wake wa kutaka Kiongozi wa Taifa Hilo Joseph Kabila kuondoka mamlakani ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
Kulingana na Chapisho hilo la ratiba ya Uchaguzi matokeo ya muda yatatangazwa katika kipindi cha wiki moja baada ya upigaji kura kufanyika, mnamo tarehe 30 Desemba, lakini matokeo kamili yatatangazwa tarehe 9 januari, 2019 na siku tatu baadae Rais Mteule Kuapishwa kushika hatamu.
Licha ya kurejesha Nyuma tarehe ya Uchaguzi Upinzani Nchini humo umeendelea kushikilia Msimamo wake wa kutaka Kiongozi wa Taifa Hilo Joseph Kabila kuondoka mamlakani ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

0 comments:
Post a Comment