Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani



Kwa habari za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiburudani

Labels

Saturday, April 14, 2018

MFAHAMU VEMA RAIS MPYA WA TLS, FATMA KARUME.

Mwanasheria mkongwe, Fatma Karume, ameshinda nafasi ya urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Fatma, ambaye licha ya kuwa mwanachama wa TLS kwa muda mrefu, lakini pia ni mtoto wa Rais wa sita wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Zoezi la kupiga na kuhesabu kura lilianza tangu asubuhi leo Aprili 14, mjini Arusha na likakamilika jioni huku Fatma akiibuka na kura  820 dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Wakili Godwin Ngwilimi, aliyepata kura 363.

Wagombea wengine wa nafasi ya urais wa TLS walikuwa ni Godwin Mwapongo aliyepata kura 12 na Godfrey Wasonga, aliyepata kura sita.

Fatma ni nani?

Fatma Karume amezaliwa Juni 15, 1969, visiwani Zanzibar,

Ni Mtoto wa rais wa sita wa Zanzibar, Amani Abeid Karume

Ni mjukuu wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Abeid Amani Karume.

Ni mwanasheria katika kampuni ya uwakili ya IMMA Advocates

Ni mwanzilishi wa kampuni ya uwakili ya Karume and Co Advocates 2004.

Fatma amewahi kuwa mwanasheria wa mwanasiasa Tundu Lissu katika kesi yake ya uchochezi, Julai mwaka jana.

Ofisi za kampuni ya uwakili ya IMMMA zilizopo Upanga, jijini hapa, ziliungua moto Agosti mwaka jana.


⧭Elimu Yake.

Degree of the Utter Bar, Middle Temple, London, 1998 Postgraduate Diploma in Professional Legal Skills, Inns of Court School of Law, 1998 LLM, London School of Economics, 1997 Diplome de Sciences Juridiques, Universite de Strasbourg, 1991 LLB (Hons), University of Sussex, 1992

0 comments:

Post a Comment