Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto
Kabwe, amekamatwa na Jeshi la Polisi asubuhi hii akiwa nyumbani kwake
jijini Dar es salaam na amepelekwa kituo cha Polisi Chang'ombe.
Taarifa
fupi iliyotolewa na Afisa habari wa Chama hicho Abdallah Khamis,
amethibitisha kukamatwa kwa kiongozi huyo huku akibainisha kwamba sababu
za kukamatwa kwake zinawezekana kuwa ni kutokana na hotuba yake
aliyoitoa juzi Oktoba 29, 2017 katika kata ya Kijichi, Mbagala Jijini
Dar es salaam katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa mdogo wa
madiwani kwenye kata 43 nchini.
0 comments:
Post a Comment