 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe 
amezindua Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ambayo yanalenga kuonyesha 
namna mashujaa wa Tanganyika walipambana kupata uhuru, maonyesho ambayo 
yatafanyika kwa muda wa mwezi mmoja katika Makumbusho ya Taifa- Nyumba 
ya Utamaduni jijini Dar es Salaam. Uzinduzi wa maonyesho hayo ambao ni 
sehemu ya utekelezaji wa Mradi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU), kwa
 lengo ya kuendeleza juhudi za Uhifadhi wa Hifadhi ya Urithi 
Tanzania,hususani ya Ukombozi wa Afrika yanasimamiwa na Shirika la Umoja
 wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Akizungumza katika 
hafla ya uzinduzi wa maonyesho hayo, Dkt. Mwakyembe alisema mradi huo wa
 kuhifadhi historia ya Ukombozi wa bara la Afrika ni muhimu kwa Tanzania
 kwani unaweza kusaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini 
kuliko ilivyo sasa kwani inawapa nafasi wageni ya kuona mambo tofauti na
 yaliyozoeleka pindi wanapokuja nchini.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe 
amezindua Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ambayo yanalenga kuonyesha 
namna mashujaa wa Tanganyika walipambana kupata uhuru, maonyesho ambayo 
yatafanyika kwa muda wa mwezi mmoja katika Makumbusho ya Taifa- Nyumba 
ya Utamaduni jijini Dar es Salaam. Uzinduzi wa maonyesho hayo ambao ni 
sehemu ya utekelezaji wa Mradi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU), kwa
 lengo ya kuendeleza juhudi za Uhifadhi wa Hifadhi ya Urithi 
Tanzania,hususani ya Ukombozi wa Afrika yanasimamiwa na Shirika la Umoja
 wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Akizungumza katika 
hafla ya uzinduzi wa maonyesho hayo, Dkt. Mwakyembe alisema mradi huo wa
 kuhifadhi historia ya Ukombozi wa bara la Afrika ni muhimu kwa Tanzania
 kwani unaweza kusaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini 
kuliko ilivyo sasa kwani inawapa nafasi wageni ya kuona mambo tofauti na
 yaliyozoeleka pindi wanapokuja nchini.  Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe 
akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na 
Mapambano ya kupata Uhuru. “Tuna mradi ambao utatupeleka mbali sana 
Watanzania, Afrika Kusini, Namibia, Angola hata wao wametuambia tusije 
shangaa sehemu hiyo ikawa inaleta watalii wengi zaidi kuliko wanaokuja 
kuangalia tembo na simba, urithi wa Afrika tumekabidhiwa na bara la 
Afrika ni wajibu wetu Watanzania kuusukuma huu mradi maana 
tumeshachelewa, Watanzania wengi labda hawaelewi mwaka 2011 kwa 
kushirikiana na UNESCO tulipeleka ombi AU la mradi huu wa bara la Afrika
 na wakaubariki huu mradi na wakaamua makao makuu yawe Tanzania na sisi 
tukachagua Dar na hapa kitajengwa kituo kikubwa kitakuwa na historia ya 
Ukombozi wa Afrika, sisi ndiyo viongozi wa huu mradi,” alisema Dkt. 
Mwakyembe. Alisema ili kufanikisha mradi huo tayari wameanza kuchukua 
hatua mbalimbali ili kuhakikisha pindi watakapojenga kituoambacho 
kitatumika kuhifadhi vitu mbalimbali ambavyo vilitumika katika kipindi 
cha ukombozi wa bara la Afrika kuwe na taarifa nyingi kuhusu bara la 
Afrika. “Tunawatumia wazee walio na historia ya ukombozi wa Afrika 
tumehoji zaidi ya wazee 100 na tunaendelea na hilo zoezi na tumebaini 
maeneo zaidi ya 200 Tanzania ambayo yanahitaji kuhifadhiwa, ni wajibu 
wangu kupeleka muswada bungeni ili tuyahifadhi na kuyalinda kwa kutumia 
sheria,” alisema Waziri Mwakyembe.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe 
akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na 
Mapambano ya kupata Uhuru. “Tuna mradi ambao utatupeleka mbali sana 
Watanzania, Afrika Kusini, Namibia, Angola hata wao wametuambia tusije 
shangaa sehemu hiyo ikawa inaleta watalii wengi zaidi kuliko wanaokuja 
kuangalia tembo na simba, urithi wa Afrika tumekabidhiwa na bara la 
Afrika ni wajibu wetu Watanzania kuusukuma huu mradi maana 
tumeshachelewa, Watanzania wengi labda hawaelewi mwaka 2011 kwa 
kushirikiana na UNESCO tulipeleka ombi AU la mradi huu wa bara la Afrika
 na wakaubariki huu mradi na wakaamua makao makuu yawe Tanzania na sisi 
tukachagua Dar na hapa kitajengwa kituo kikubwa kitakuwa na historia ya 
Ukombozi wa Afrika, sisi ndiyo viongozi wa huu mradi,” alisema Dkt. 
Mwakyembe. Alisema ili kufanikisha mradi huo tayari wameanza kuchukua 
hatua mbalimbali ili kuhakikisha pindi watakapojenga kituoambacho 
kitatumika kuhifadhi vitu mbalimbali ambavyo vilitumika katika kipindi 
cha ukombozi wa bara la Afrika kuwe na taarifa nyingi kuhusu bara la 
Afrika. “Tunawatumia wazee walio na historia ya ukombozi wa Afrika 
tumehoji zaidi ya wazee 100 na tunaendelea na hilo zoezi na tumebaini 
maeneo zaidi ya 200 Tanzania ambayo yanahitaji kuhifadhiwa, ni wajibu 
wangu kupeleka muswada bungeni ili tuyahifadhi na kuyalinda kwa kutumia 
sheria,” alisema Waziri Mwakyembe.  Balozi
 wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer akizungumza 
katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata
 Uhuru. Kwa upande wa Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), 
Roeland Van de Geer alisema ni muhimu kwa bara la Afrika kuwa na 
maonyesho ambayo yanaelezea historia ya bara hilo ili yatumike kuelezea 
kizazi cha sasa na kijacho namna nchi za Afrika zilipambana kupata uhuru
 na wao kama EU wataendelea kusaidia miradi mbalimbali yenye lengo ya 
kutunza urithi wa bara la Afrika. “Ni jambo la kujivunia kwa Umoja wa 
nchi za Ulaya kusaidia kufanikisha mradi huu … EU tumekuwa tukisaidia 
miradi mingi na hii yote ni kwa ajili ya kutunza utamaduni na urithi wa 
bara la Afrika, tumesaidia miradi mbalimbali nchini ikiwepo ya Olduvai 
na Ngorongoro na tutaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania 
kuendeleza maeneo ya kihistoria,” alisema.
Balozi
 wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer akizungumza 
katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata
 Uhuru. Kwa upande wa Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), 
Roeland Van de Geer alisema ni muhimu kwa bara la Afrika kuwa na 
maonyesho ambayo yanaelezea historia ya bara hilo ili yatumike kuelezea 
kizazi cha sasa na kijacho namna nchi za Afrika zilipambana kupata uhuru
 na wao kama EU wataendelea kusaidia miradi mbalimbali yenye lengo ya 
kutunza urithi wa bara la Afrika. “Ni jambo la kujivunia kwa Umoja wa 
nchi za Ulaya kusaidia kufanikisha mradi huu … EU tumekuwa tukisaidia 
miradi mingi na hii yote ni kwa ajili ya kutunza utamaduni na urithi wa 
bara la Afrika, tumesaidia miradi mbalimbali nchini ikiwepo ya Olduvai 
na Ngorongoro na tutaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania 
kuendeleza maeneo ya kihistoria,” alisema.  Afisa
 Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege akizungumza katika hafla ya 
uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru. Naye 
Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki na Afisa Mwakilishi
 wa Unesco Dar, Ann Therese Ndong- Jatta katika hotuba yake iliyosomwa 
na Afisa Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege alisema ni jambo zuri
 kuwepo na makumbusho ambayo yanaeleza historia ya bara la Afrika na 
yatawza kuwapa nafasi watu mbalimbali kutoka mataifa ya nje ya bara la 
Afrika kuona na kujifunza historia ya Afrika. “Makumbusho haya ni muhimu
 kwasababu ni sehemu ya ukumbusho wetu kwa baadae, kupitia makumbusho 
haya tutaona historia ya bara la Afrika, historia ya mwanadamu na safari
 ya kutafuta uhuru ilivyokuwa,” alisema Kaizilege.
Afisa
 Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege akizungumza katika hafla ya 
uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru. Naye 
Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki na Afisa Mwakilishi
 wa Unesco Dar, Ann Therese Ndong- Jatta katika hotuba yake iliyosomwa 
na Afisa Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege alisema ni jambo zuri
 kuwepo na makumbusho ambayo yanaeleza historia ya bara la Afrika na 
yatawza kuwapa nafasi watu mbalimbali kutoka mataifa ya nje ya bara la 
Afrika kuona na kujifunza historia ya Afrika. “Makumbusho haya ni muhimu
 kwasababu ni sehemu ya ukumbusho wetu kwa baadae, kupitia makumbusho 
haya tutaona historia ya bara la Afrika, historia ya mwanadamu na safari
 ya kutafuta uhuru ilivyokuwa,” alisema Kaizilege.  Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na 
Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer 
wakikata utepe katika uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya 
kupata Uhuru.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na 
Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer 
wakikata utepe katika uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya 
kupata Uhuru. Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa 
ameongozana na Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van
 de Geer na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuangalia vitu 
mbalimbali vya kihistoria ambavyo vimewekwa katikaMaonyesho ya Mashujaa 
na Mapambano ya kupata Uhuru.
 Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa 
ameongozana na Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van
 de Geer na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuangalia vitu 
mbalimbali vya kihistoria ambavyo vimewekwa katikaMaonyesho ya Mashujaa 
na Mapambano ya kupata Uhuru.

 
@MICHUZIJR
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment