Rais John Magufuli ameanza ziara
rasmi ya kiserikali ya siku tatu nchini Uganda kwa mwaliko wa Rais
Yoweri Museveni.
Dk Magufuli aliyeongozana na mkewe
Janeth amewasili Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda ambako amepokewa
na mwenyeji wake Rais Museveni aliyeambatana na mkewe Janeth.
Katika
mapokezi hayo leo Alhamisi Novemba 9,2017, Rais Magufuli amepigiwa
mizinga 21 na amekagua gwaride lililoandaliwa kwa heshima yake.
Wakiwa mpakani, viongozi hao wawili watafungua kituo cha pamoja cha huduma za mpakani (One Stop Border Post - OSBP) kilichojengwa ili kurahisisha utaratibu wa forodha, uhamiaji na kuharakisha biashara kati ya nchini hizi mbili.
Taarifa
ya Ikulu imesema baadaye leo, marais hao wataweka jiwe la msingi katika
mradi wa bomba la mafuta ghafi linaloanzia Hoima nchini Uganda hadi
Bandari ya Tanga nchini Tanzania.
Shughuli hiyo itafanyika katika Kijiji cha Luzinga, kilichopo mkoani Rakai nchini Uganda.
Baada
ya ufunguzi, viongozi hao watazungumza na wananchi katika mkutano wa
hadhara utakaofanyika wilayani Kyotera nchini Uganda.
Rais Magufuli jioni ya leo atahudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima yake na Rais Museveni katika mji wa Masaka. @MCL.
0 comments:
Post a Comment