Mpina alitangaza hayo leo Jumatatu bungeni mjini Dodoma wakati akichangia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa 2018/2019.
Waziri
huyo ambaye alikuwa akijibu hoja zilizoibuliwa na baadhi ya wabunge
amesema ng'ombe hao watapigwa mnada wakati wowote kama ilivyofanya kwa
ng'ombe 1,325 wa Kenya.
Amesema uhusiano wa Tanzania
nchi nyingine washirika wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ni mzuri na
akisisitiza hakuna ushirikano wa kihalifu.
Mpina
amesema walioingiza ng'ombe hao ni wahalifu na wamevunja sheria za nchi
na kutahadharisha wafugaji wa nchi jirani kufuata sheria wanapotaka
kuingiza mifugo nchini.
By Daniel Mjema, Mwananchi
By Daniel Mjema, Mwananchi
0 comments:
Post a Comment