22 Januari 2018,
Katika kampeni za
uchaguzi mdogo Jimbo la Siha Kata ya Ngarenairobi, Katibu wa NEC,
Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole, amewaeleza wananchi wa Jimbo
la Siha kuwa kuichagua CCM ni kuchagua maendeleo ya watu wa Jimbo la
Siha.
Kampeni za kumnadi
mgombea Ubunge wa CCM, zimehudhuriwa na umati wa wananchi wa wilaya ya
Siha na Viongozi wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti Mkoa wa Kilimanjaro
Ndg. Patrick Peter Boisafi.
Katibu Mwenezi wa CCM
amewaeleza wananchi, CCM inazifahamu changamoto za Jimbo la Siha ikiwa
ni pamoja na suala la Ardhi, Huduma za afya na Suala la Shule ya Msingi
na Sekondari. Hivyo CCM ipo tayari kuzitatua changamoto hizo kwa wakati
baada ya timu ya kuleta maendeleo kukamilika endapo wananchi wa Jimbo
la Siha watamchagua kwa kura nyingi Dr Godwin Mollel kuwa Mbunge wa Siha
kwa tiketi ya CCM.
*Baada ya Dr. Mollel
kutazama na kuona maendeleo yanacheleweshwa na Chama chake cha awali
(Chadema) ambacho hakina dira wala muelekeo, Dr Mollel ameamua kujumuika
na timu ya ushindi, waheshimiwa wananchi mchagueni Dr Mollel awatumikie
,awahudumie na awaletee maendeleo. Lazima ifike wakati tunapomtafuta
mwakilishi ambaye anakwenda kuwawakilisha wananchi, tupate mwakilishi
ambaye akiwatazama usoni anajua shida na changamoto zenu*. Amesema Ndg.
Polepole.
Katika mkutano huo
wananchi wameelezwa juu ya tabia za vyama vya upinzani kukosa msimamo
katika kusimamia agenda za wananchi na kuwasihi kutovichagua vyama
hivyo. *Chama kisicho kuwa na msimamo hakipaswi kupewa dhamana yoyote ya
uongozi. Walisema hatuna shirika la ndege, walisema kuhusu baadhi ya
watu ni mafisadi, walisema Rais asisafiri kwenda nje ya nchi, walisema
kuhusu madini na sasa tunaye Ndg. Magufuli anayechukizwa na rushwa na
kila aina ya ubadhirifu wa mali za umma, anatenda sawasawa na matakwa ya
wananchi wa Tanzania lakini wapinzani sasa wanasema kinyume na kupinga
kila jema*. Amesisitiza Ndg. Polepole.
Huu ni muendelezo wa
ziara za Katibu Mwenezi wa CCM zenye lengo la kujenga Chama pamoja na
kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM 2015-
2020.
Imetolewa na,
*IDARA YA ITIKADI NA UENEZI*
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
SIHA, KILIMANJARO
0 comments:
Post a Comment