Na Ali Issa Maelezo
Mswada wa sheria ya kuazisha
Bima ya afya kazini kwa watumishi wa Umma Zanzibar tayari umepitishwa
kwenye kamati ya makatibu wakuu na baraza la Mapinduzi Zanzibar .
Hayo yamesemwa leo huko baraza la
wawakilishi nje kidogo ya mji wa Zanzibar katika kikao kinacho endele
na waziri wa kazi,uwezeshaji,wazee ,vijana,wanawake na watoto Moudline
Cyrus Castico wakati akijibu maswali ya Ripoti ya ufafanuzi wa ushauri
uliotolewa na kamati ya maendeleo ya wanawake, habari na utalii ya
Baraza la wakilishi.
Amsema mswada huwo wa Sheria wa
kuazishwa bima hiyo kwa wafanya kazi wa umma sasa hivi upo katika ofisi
ya mwanasheria mkuu wa Zanzibar kufanyiwa marekebisho yanayo stahiki na
hatimae utawasilishwa baraza la wakilishi.
Amesema hatua imekuja badayakuona
kuwa wafanya kazi wanafanya kazi muda mwingi na kupatwa na matatizo
mbali mbali ya kiafya jamboamalo kwa ghafla wafanya kazi hushindwa
kujitibu hivyo bima hiyo kwa wajiriwa ni muafaka kwao kwani itawasaidia
kujitibu maradhi, majanga ya ajali kazini na kupata matibabu ya uhakika
pale tokeo limetokea.
Amsema hali hiyo itawasaidia
wafanyakazi kuona kuwa wanajaliwa na watumishi wao kwani wao ni
watumishi na waleta wamaendeleo kwa Taifa lao.
Akizingatia ushauri huo wa ripoti
hiyo suala la afya ya usalama kazini waziri huyo alisema wizara
kupitia idara ya usalama na afya kazini idara inaendelea kufanya ukaguzi
kwenye sehemu za kazi ili kuona wafanya kazi wanafanya kazi katika hali
ya usalama na kupatiwa vifaa vya kinga kulingana na kazi yake.
Alisema katika kusimamia suala
hilo kwa ufanisi,idara imetayarisha rasimu za kanuni zitakazo wabana
wajiri na wajiriwa kutekeleza suala hilo kwa mujibu wa kifungu cha
sheria 116(1) na (2) cha sheria ya usalama na afya kazini namba 8ya
mwaka 2005.
Hata hivyo alisema wizara imefanya ukaguzi wa usalama kazini mwaka 2016-17katika taasisi 139 kwa unguja na pemba.
Alitaja maeneo walipita ni pamoja
na viwanda ,taasisi za ujenzi mahoteli na vituo vya mafuta,ambapo kila
tassisi ilielezwa vifaa vya kununua kwa ajili ya kuwakinga
wafanyakaziwao kwa mujibu wa kazi wanazo fanya.
Wakati huohuo waziri huyo
aliwahidi vijana wale wote wa Zanzibar waliopo katika mabaraza ya vijana
wanao hitaji mikopo na wanao kidhi vigezo vinavyo hitajika watapatiwa
mikopo bila ya usumbufu wowote.
Amesema kutokana na uzowefu walio
nao katika mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi ,unaosimamiwa na
wizarayake hilo linawezekana kwa wale waliopo katika mabaraza.
0 comments:
Post a Comment