Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) linasikitika kutangaza vifo vya Askari wake wawili
Koplo Maselino Paschal Fabusi na Praiveti Venance Moses Chimboni,
ambao walikuwa katika Ulinzi wa Amani nchini DRC.
Askari hao wamefariki baada ya
kushambuliwa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi tukio ambalo limetokea
tarehe 09 Octoba 2017 umbali wa kilomita 24 mashariki mwa mji wa Beni.
Majeshi yetu yamefanikiwa kuwarudisha nyuma waasi hao na kudhibiti eneo
hilo.
Kufuatia shambulizi hilo Umoja wa
Mataifa umeunda Bodi ya Uchunguzi kuchunguza tukio hilo.
Aidha, Maafisa
na Askari wa JWTZ wanaendelea kutekeleza majukumu yao katika
Operesheni hiyo.
Umoja wa Mataifa unaandaa
utaratibu wa kuleta miili ya marehemu nchini.
Mtajulishwa taratibu za
mapokezi, kuaga miili ya marehemu hao na mazishi.
Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi Amina.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
10 Octoba, 2017
0 comments:
Post a Comment